Kikosi cha kimataifa kitachoongozwa na Kenya nchini humo (MSS) na Polisi wa Kitaifa wa Haiti (PNH) wanamtaka kiongozi wa genge nchini humo Jimmy "Barbecue" Cherizier na kundi lake kujisalimisha.

Vikosi hivyo vilisema kuwa vimedumisha operesheni katika sehemu za Port-au-Prince vikilenga ngome za magenge hayo.

"MSS inatoa onyo kali kwa viongozi wa magenge: wajisalimishe sasa au wakabiliane na nguvu zisizoepukika ambazo zitawapata mapema kuliko ilivyotarajiwa," ilisema taarifa ya MSS.

Vikosi hivyo viliendelea na operesheni dhidi ya genge hilo siku ya Jumatatu, ambayo ilifichua kuwepo kwa Barbecue akiandamana na takriban wanachama 30 wa genge hilo.

"Walikuwa wakijaribu kusonga mbele katika vikundi viwili vya wanachama wapatao 15 kila moja, wakilenga Delmas 2 na 6."

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

"Vikosi vya MSS/PNH vilijibu upesi kwa nguvu za zana zinazolingana, na kuwalazimisha washiriki wa genge hilo kurudi nyuma kwa mshtuko," vikosi hovyo vilisema.

Maafisa hao waliongeza kuwa majeruhi kadhaa waliripotiwa miongoni mwa wanachama wa genge hilo na kwamba baadhi walisita kutii amri kutoka kwa anayejiita kiongozi wao, kukataa makabiliano na MSS/PNH.

MSS na HNP waliendelea na doria za usiku na mchana katika maeneo ya Carrefour paye, Route coloniale, Bois dutre jette, Fosse cheval, Alee nan parent, Ale pe josephat, Villard, Lestere na Liancourt.

Taarifa hiyo ilisema timu hiyo iliungana na wenyeji kujaza mashimo kwenye barabara ya Route Coloniale. katika Carrefour Paye, ambayo imekuwa vigumu kuitumia kwa wakulima kusafirisha mazao yao ya shambani.

Kamishna wa Gonaives alifika baadaye na msafara wake, ambapo MSS /HNP walijiunga kumsindikiza hadi Liancourt.


Hii ilisababisha kutumwa kwa maafisa wa polisi na kufunguliwa kwa kituo cha polisi cha Liancourt, ambacho kilikuwa kimetelekezwa kutokana na uvamizi wa magenge.

Wakazi walipongeza mpango wa kufungua tena Kituo cha Polisi cha Liancourt, wakiona kwamba hilo limetekelezwa kupitia uhusiano wa kikazi kati ya MSS na HNP.

Waliingia katika shangwe huku Kamishna wa Polisi wa Gonaive akikata mkanda unaoashiria kufunguliwa rasmi kwa kituo cha polisi.

Kwa kuonyesha shukrani, wenyeji walijipanga na kuanza kusafisha eneo hilo ili liwe na makazi.

Sehemu za Haiti zinakabiliwa na kuongezeka kwa mashambulizi kutoka kwa magenge huku kukiwa na hali ya sintofahamu ya kisiasa.

Polisi wa Kenya pamoja na wale kutoka Jamaica, Bahamas na Belize, wako katika nchi hiyo ya Caribbean kusaidia kupambana na magenge hayo.

Viongozi wa Haiti wameomba kuundwa kwa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa, na Baraza la Kudumu la Umoja wa Mataifa ya Marekani lilipitisha azimio mnamo Novemba 13 yenye kichwa "Katika Kuunga Mkono Ombi la Haiti la Operesheni ya Kulinda Amani ya Umoja wa Mataifa."

Waziri Mkuu wa Haiti Alix Didier Fils-Aimé Jumatatu alizindua mpango mkubwa wa kuwasaidia watu waliokimbia makazi yao katika eneo la mji mkuu wa Port-au-Prince. Ikiungwa mkono na Benki ya Maendeleo ya Marekani (IDB), hatua hii inalenga kukidhi mahitaji ya dharura ya maelfu ya watu.