
UGOMVI baina ya Harmonize na Diamond kuhusu ni nani
atakuwa wa kwanza kupeleka muziki wa Bongo Fleva hadi kwenye jukwaa la
kimataifa ungali mbali sana na kufikia kikomo.
Hii ni baada ya Harmonize kumpiga kijembe Diamond
kuhusu kutoteuliwa kuwania tuzo ya Grammy mwaka huu licha ya kuonekana kufanya
ngoma zilizotambulika kimataifa.
Akizungumza na waandishi wa habari, Harmonize
alipoulizwa kuhusu Grammy, alisema atakuwa msanii wa kwanza Afrika Mashariki
kushinda tuzo hiyo maarufu kwenye Sanaa ya muziki duniani.
Katika kile kilichoonekana kama ni kutupa kijembe kwa
Diamond katika wimbo wake wa Komasava – ambayo ni njia ya kumtaka mtu salamu
kwa lugha ya Kifaransa, Harmonize alidai kwamba wimbo huo haukuwa na maudhui
yoyote ya kumwenzesha kushinda Grammy zaidi ya salamu tu.
Kwa mujibu wa Harmonize, Diamond asingefanikiwa hata
kidogo kushinda Grammy kwa kutamka salamu kwa lugha ya Kifaransa (comment ca va)
kwenye wimbo mzima wa Komasava.
“Kuzungumzia
kuhusu Grammy, jibu langu litakuwa hivi: kama unazungumza kuhusu Grammy basi
jua hapa mnazungumza na mshindi wa Grammy Makala ya 2025/2026. Kwa sababu mimi
najua inahitaji nini ili kushinda. Huwezi shinda Grammy kwa kusalimia watu. Huwezi,”
Harmonize alisema.
“Unahitaji
utunzi na uzalishaji wa kipekee ili kushinda Grammy, halafu usichokijua ni
kwamba wnaaoandaa Grammy hata hawajui kama wewe ni maarufu, hawajui kama
unajulikana. Hivyo tujikite katika muziki, muziki wenyewe ukutangaze. Mengine hayana
maana, umaarufu kwenye makamera ni vyako tu, lakini wale wanasikiliza kazi yako
tu,” Harmonize aliongeza huku akisisitiza kwamba sharti
awepo kwenye orodha ya wawaniaji wa tuzo hizo mwakani.
Akionyesha kutyumbishwa na uwezekano finyu wa
kuteuliwa, Harmonize alisema kwamba atakuwa si tu msanii wa kwanza kutoka
Afrika Mashariki kuteuliwa kuwania Grammy lakini pia ataibuka mshindi na kurudi
na ushindi Bongo.
Kauli yake kuhusu Grammy inajiri siku chache tu baada
ya Diamond kutoa kauli yake kuhusu kutoteuliwa kuwania tuzo hizo mwaka huu
licha ya ngoma yake ya Komasava aliyomshirikisha mkali kutoka Kanada, Jason
Derulo kuonekana kuwavutia mashabiki wengi kutoka pembe nne za dunia.
Akijibu mashabiki wake walioonekana kusawijika nyuso
kwa kukosa kuliona jina lake kwenye orodha ya wawaniaji, Diamond alisema kwamba
mashabiki hawafai kukata tamaa, bali wanafaa kumpa moyo kutumia hiyo kama funzo
kujiboresha zaidi katika uteuzi wa mwaka ujao.
“Tunapofeli
kufanikiwa tusichukie, lazima tuongeze kasi na kuifanyia tathmini kuangalia ni
sehemu gani tuliteleza,” Diamond alisema.
‘Mimi ni miongoni mwa watu tukikaa na timu yangu tusipochukua kitu chochote hatujakipata. Wakianza kulalamika sipendi. Nawaambia pale huenda kuna sehemu hatuko sawa. Pengine hatuna connection, au kuna dosari katika kazi yetu tuliyoifanya,’ aliongeza.
Diamond aliahidi kuzama kwenye studio kwa mara
nyingine tena kujibidiisha katika kutoa ngoma kali alizozirejelea kama ‘mawe’
ili kuboresha nafasi yake ya kuwepo kwenye orodha ya wawaniaji wa Grammy mwaka
ujao, na pengine hata kuibuka na ushindi.
“Kwa sasa hivi ni kumwaga mawe [nyimbo] mengi sana duniani. Mwenyezi Mungu atatuandikia mwakani tunaingia [Grammy] na kama hatuingii tutafika kwa pamoja ama tunaungama kwa sababu mimi naamini kwamba hakuna kisichowezekana,” alisema.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!