
MIEZI kadhaa baada ya malkia wa muziki wa kizazi
kipya kutoka Kameruni, Sabrina kuachia albamu yake ya ‘Unstoppable’, mrembo
huyo amerejea tena na kolabo nyingie ya nguvu na D Smoke.
Baada ya miezi 7 ya ladha ya kipekee ya albamu ya
Unstoppable kuteka maskio ya wapenzi wa muziki wa Kiafrika, Sabrina safari hii
ameibuka na ngoma kwa jina ‘Pull Over’ akimshirikisha D Smoke – msanii aliyejizolea
umaarufu baada ya kuteuliwa kuwania tuzo ya kifahari ya Grammy.
Akizungumzia kuhusu ujio wa ngoma hiyo yenye mtindo
wa Amapiano, Sabrina anasema kwamba ni ngoma yenye ladha ya kipekee inayonuia
kutia mshawasha katika nyoyo za wapenzi wa muziki si tu barani Afrika bali kote
duniani.
“Wimbo
huu wenye kichocheo cha Amapiano unatazamiwa kuangazia mawimbi ya kimataifa,
ukichanganya midundo ya Kiafrika na misatari ya kipekee,’
alisema.
Wimbo wa ‘Pull Over’ unaonyesha mtindo wa sahihi wa
Sabrina, unaounganisha kwa wepesi usuli wake wa Kikameruni na mvuto wa kisasa
wa kimataifa.
Sauti zake kuu zilizooanishwa na mistari madhubuti ya
D Smoke vimeunda wimbo wenye nguvu, unaojikita katika aina ambayo inazungumza
kuhusu uthabiti, muunganisho na lugha ya muziki ya ulimwengu wote.
"Kushirikiana
na D Smoke kwenye PULL OVER kumekuwa tukio la kushangaza,"
Sabrina alisema.
"Wimbo huu unahusu kutafuta umoja katika utofauti na kusherehekea uzuri wa ulimwengu tofauti ujao pamoja.”
Kwa upande wake, D Smoke alikiri kuwa kufanya kazi na
Sabrina kulikuwa moja la tukio la kupendeza sana, kwani alihisi uwepo wa
talanta tupu katika sauti ya mrembo huyo.
“Kufanya kazi na Sabrina kulitia moyo. Nguvu na usanii wake haulinganishwi, na mimi nina furaha kwa ulimwengu kuhisi upekee ambao tumeunda."
Wimbo huu unaambatana na video mahiri ya muziki
ambayo huboresha mada za wimbo huo kwa kuvutia picha, kusherehekea kiini cha
Amapiano na utamaduni wa hip-hop.
Sabrina ni msanii chipukizi kutoka Cameroon
anayefafanua upya tasnia ya muziki ya kimataifa kwa mchanganyiko wake wa
kipekee wa Amapiano, nafsi, na sauti za kisasa.
Anafahamika zaidi kwa albamu yake ya Unstoppable
ambayo aliiachia mwezi Aprili mwaka huu na kumtangaza vyema kote barani Afrika.
Kwa upande mwingine, D Smoke ni rapa kutoka Marekani
ambaye alipata umaarufu baada ya kuibuka mshjindi kwenye Rhythm + Flow ya
Netflix na kisha baadae akajinafasi katika orodha ya walioteuliwa kuwania tuzo
za Grammy.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!