Mechi ya Ligi Kuu ya Kenya baina ya Mara Sugar na Sofapaka


Mara Sugar ilifunga bao katika dakika za lala salama na kuzoa alama muhimu nyumbani dhidi ya Sofapaka kwenye mechi iliyokuwa na ushindani mkali katika uwanja wa Awendo Green, Migori mnamo Jumapili.

Ronald Sempala aliweka Batoto Ba Mungu mbele dakika ya nne kupitia usaidizi wake Baron Ochieng.

Mara Sugar, hata hivyo, walisawazisha katika dakika ya tano ya muda ulioongezwa kupitia mkwaju wa faulo, huku mchezaji bora wa mechi Matthias Isogol akipachika wavu.

Matokeo hayo yaliifanya Mara kupunguza uongozi wa KCB hadi pointi nne, huku Sofapaka, ambayo sasa haijafungwa katika mechi tano za mwisho baada ya kuanza vibaya, iliruka hadi nambari tisa.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Mara Sugar, haikuwa na mkufunzi wao nkuu George Midenyo ambaye alipokea kadi nyekundu wakati wa mechi yao dhidi ya AFC Leopards juma lililopita.