
Takriban watu watano wamefariki katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu eneo la Kagocho kati ya Karatina na Sagana, Kaunti ya Kirinyaga.
Msemaji wa polisi Dkt Resila Onyango alisema ajali hiyo ilitokea Ijumaa asubuhi na ilihusisha trela ambalo liligonga magari.
"Watu watano walikufa papo hapo huku idadi isiyojulikana ya wengine wakijeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali tofauti," alisema.
Aliongeza kuwa polisi wanachunguza tukio hilo. Lori lililokuwa likielekea Sagana lililokuwa likisafirisha magunia ya mahindi lilishindwa kulidhibiti na kugonga magari mawili ya kibinafsi yaliyokuwa yakielekea Karatina.
Lori hilo lilipinduka likiwa katika mwendo kasi na kumwaga magunia kadhaa ya mahindi barabarani.
Baadhi ya wenyeji waligombania chakula hicho.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!