Wachezaji watatu wa Kenya Emmanuel Wanyonyi, Faith Kipyegon na Beatrice Chebet wameteuliwa kuwania tuzo za mwanariadha bora wa mwaka wa Riadha wa Dunia.

Wanyonyi, bingwa wa Olimpiki wa mbio za mita 800, anawania tuzo ya mwanariadha bora wa mwaka wa mbio za kiume ambapo anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa bingwa wa Olimpiki wa mbio za mita 400 Rai Benjamini (Marekani), na wengine

Wakati huo huo, kitengo cha wanawake kinawakutanisha Kipyegon na Chebet dhidi ya orodha iliyojaa nyota inayojumuisha bingwa wa Olimpiki wa mita 100 Julian Alfred wa St Lucia, Sydney McLaughlin-Levrone wa Marekani na wengine.