Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai imemuagiza Naibu Rais aliyetimuliwa Rigathi Gachagu kurekodi taarifa kuhusu madai kuwa kumekuwa na majaribio ya kumuua.

 

DCI, katika taarifa yake, alitaja madai ya Gachagua kuwa mazito na ambayo hayawezi kuchukuliwa kirahisi.

"Haya ni madai mazito yanayotoka kwa mtu wa hadhi yako na hayawezi kuchukuliwa kirahisi," Ofisi ya DCI ilisema katika taarifa iliyotiwa saini na J.K Marete.

Kwa kuzingatia uzito wa suala hili, tunaomba uwepo wako mnamo tarehe 22 Oktoba 2024 katika makao makuu ya Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai, Mazingira Complex-Kiambu. Road, kurekodi taarifa yako ili kuwezesha uchunguzi wa haraka na wa kina kuhusu suala hilo," ilielekeza DCI.

'Tunaelewa unyeti wa madai hayo na tunakuhakikishia kuwa suala hili litashughulikiwa kwa uzito unaostahili. Kauli yako ni sehemu muhimu ya uchunguzi wetu," DCI ilisema.

Siku ya Jumapili, Gachagua alidai kuwa kulikuwa na majaribio mawili ya kumuua ambayo hayakufaulu kabla ya mpango wa kumuondoa madarakani kutekelezwa.Akizungumza baada ya kuruhusiwa kutoka katika hospitali ya Karen, Gachagua alisema kuondolewa ofisini kwake kulikuja baada ya majaribio ya mauaji ya vyombo vya usalama kufeli.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Gachagua alibainisha kuwa jaribio la kwanza lilikuwa Kisumu mwishoni mwa Agosti ambapo aliwekewa sumu kwenye chakula chake kabla ya timu yake kugundua.

"Mnamo Agosti 30, huko Kisumu, maafisa wa usalama waliofichwa waliingia chumbani kwangu na kukivamia na mmoja wao akajaribu kutia sumu kwenye chakula changu, lakini tuligundua na tukaweza kutoroka mpango huo. Ilipangwa niuawe kwa sumu ya chakula, " Gachagua alisema.

Mwanasiasa huyo alidai kuwa jaribio la pili la mauaji lilijiri siku chache baadaye katika kaunti ya Nyeri na lilitekelezwa na Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi.

“Mnamo Septemba 3, timu nyingine kutoka Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi ilifika Nyeri na kujaribu kutia sumu kwenye chakula ambacho kilikusudiwa mimi na baraza la wazee wa Kikuyu,” alisema.

Aliongeza, "Niliripoti suala hili kwa NIS na kuwataka maafisa waliopewa kazi katika afisi yangu kuondoka kwa sababu nilihisi siko salama. Baada ya majaribio hayo mawili ya mauaji kufeli, ndipo hoja hii ya kunitimua ilipoasisiwa.”