Siku ya Jumapili asubuhi, naibu wa rais aliyetimuliwa Rigathi Gachagua alizamia kwenye mitandao ya kijamii kutuma salamu zake kwa Wakenya huku taifa likiadhimisha Siku ya Mashujaa.

Katika taarifa yake fupi kuhusu mtandao wa X, mwanasiasa huyo ambaye hivi majuzi alipoteza kiti chake cha naibu rais baada ya seneti kuidhinisha mashtaka kadhaa yaliyotolewa dhidi yake aliwatakia Wakenya sikukuu njema ya Mashujaa.

Gachagua pia alisema dua kwa Kenya huku akiomba Mungu abariki taifa hili.

“Heri ya Sikukuu ya Mashujaa wapendwa Wakenya. Mungu abariki taifa letu,” Gachagua alisema Jumapili asubuhi.

Haya yanajiri takriban siku mbili tu baada ya mbunge huyo wa Mathira kuondolewa kutoka katika kiti chake cha naibu rais na bunge la seneti.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Maseneta wa Kenya mnamo siku ya Alhamisi usiku waliunga mkono kuondolewa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua.

Maseneta waliidhinisha mashtaka matano kati ya 11 yaliyotolewa dhidi ya Gachagua.

"Seneti imeazimia kumuondoa afisini kwa kumwondoa madarakani MHE. Rigathi Gachagua, Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya. Kwa hiyo, H.E. Rigathi Gachagua akoma kushikilia wadhifa huo,” Spika Amason Kingi alisema.

Mashtaka yaliyoidhinishwa ni pamoja na; shtaka la maoni ya Wanahisa, mashtaka manne ya kuingilia Uhuru wa Majaji na mashtaka matano ya Sheria ya Uwiano na Uadilifu wa Kitaifa.

Pia walishikilia misingi ya sita na tisa kuhusu uhalifu chini ya Sheria ya Uwiano wa Kitaifa na Utovu wa Maadili Mkubwa. 

Siku ya Ijumaa, Bunge la kitaifa lilipiga kura kuidhinisha utezi wa Kithure Kindiki kuwa naibu wa rais.

Hii ilikuwa ni baada ya wabunge 236 kupiga kura kuidhinisha uteuzi uliyofanywa na rais William Ruto akimpendekeza Kindiki kuwa naibu Rais siku ya Ijumaa.

Hatua hii sasa ilimaanisha kuwa rais Ruto anaweza wakati wowote kumteua rasmi Kindiki kuwa naibu rais kuchukua nafasi ya Rigathi Gachagua.

Baada ya uteuzi rasmi, naibu rais mteule aliratibiwa kuapishwa katika hafla ambayo ingeshuhudiwa na jaji mkuu.

Mahakama hata hivyo ilisimamisha kuapishwa kwa Kindiki kama naibu kuinua mpya huku mbili zilizowasilishwa zikisubiri kusikilizwa.