Siku
ya Jumapili asubuhi, naibu wa rais aliyetimuliwa Rigathi Gachagua alizamia
kwenye mitandao ya kijamii kutuma salamu zake kwa Wakenya huku taifa
likiadhimisha Siku ya Mashujaa.
Katika
taarifa yake fupi kuhusu mtandao wa X, mwanasiasa huyo ambaye hivi majuzi
alipoteza kiti chake cha naibu rais baada ya seneti kuidhinisha mashtaka kadhaa
yaliyotolewa dhidi yake aliwatakia Wakenya sikukuu njema ya Mashujaa.
Gachagua
pia alisema dua kwa Kenya huku akiomba Mungu abariki taifa hili.
“Heri
ya Sikukuu ya Mashujaa wapendwa Wakenya. Mungu abariki taifa letu,” Gachagua
alisema Jumapili asubuhi.
Haya
yanajiri takriban siku mbili tu baada ya mbunge huyo wa Mathira kuondolewa
kutoka katika kiti chake cha naibu rais na bunge la seneti.
Maseneta wa Kenya mnamo siku ya Alhamisi usiku waliunga mkono kuondolewa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua.
Maseneta waliidhinisha mashtaka matano kati ya 11 yaliyotolewa dhidi ya Gachagua.
"Seneti imeazimia kumuondoa afisini kwa kumwondoa madarakani MHE. Rigathi Gachagua, Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya. Kwa hiyo, H.E. Rigathi Gachagua akoma kushikilia wadhifa huo,” Spika Amason Kingi alisema.
Mashtaka yaliyoidhinishwa ni pamoja na; shtaka la maoni ya Wanahisa, mashtaka manne ya kuingilia Uhuru wa Majaji na mashtaka matano ya Sheria ya Uwiano na Uadilifu wa Kitaifa.
Pia walishikilia misingi ya sita na tisa kuhusu uhalifu chini ya Sheria ya Uwiano wa Kitaifa na Utovu wa Maadili Mkubwa.
Siku
ya Ijumaa, Bunge la kitaifa lilipiga kura kuidhinisha utezi wa Kithure Kindiki
kuwa naibu wa rais.
Hii
ilikuwa ni baada ya wabunge 236 kupiga kura kuidhinisha uteuzi uliyofanywa na
rais William Ruto akimpendekeza Kindiki kuwa naibu Rais siku ya Ijumaa.
Hatua
hii sasa ilimaanisha kuwa rais Ruto anaweza wakati wowote kumteua rasmi Kindiki
kuwa naibu rais kuchukua nafasi ya Rigathi Gachagua.
Baada
ya uteuzi rasmi, naibu rais mteule aliratibiwa kuapishwa katika hafla ambayo
ingeshuhudiwa na jaji mkuu.
Mahakama
hata hivyo ilisimamisha kuapishwa kwa Kindiki kama naibu kuinua mpya huku mbili
zilizowasilishwa zikisubiri kusikilizwa.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!