Mwanaharakati maarufu wa kisiasa na wakili David Morara
Kebaso alikumbana na kizingiti katika ziara yake ya Siku ya Mashujaa katika kaunti ya Narok baada ya watu wasiojulikana
kudaiwa kuwashambulia.
Kulingana
na kiongozi huyo wa chama cha INJECT, mwanasiasa mkubwa wa Narok ambaye jina
lake halikutajwa alituma wahuni kumshambulia yeye na timu yake mnamo siku ya
Jumamosi walipokuwa wakizuru kaunti hiyo.
Morara alisema kuwa zaidi ya washambuliaji 50 walitumwa kwao na mwanasiasa huyo ambaye hakutajwa jina kwa lengo la kumzuia kufichua ukweli.
"Walipotoroka watu zaidi ya 50 ambao ulikuwa umewakodi kuziba barabara, majambazi wako walitufuata kwa magari mawili (prado na pickup nyeupe) na wanaweza kuonekana wakitushambulia," Morara alisema chini ya video ya shambulio hilo ambayo alichapisha.
Wakili huyo aliendelea kudai kuwa baadhi ya wanachama wa timu yake walikamatwa na kupigwa baada ya tairi la gari lao kupasuka.
“Tairi la gari letu lilipopasuka na lingine kuondoka barabarani, Wakenya hawa wasio na hatia walitelekeza magari hayo na kukimbia kwa miguu, walionaswa walipigwa katika jaribio la kuwaua. Haina mambo baba, leo ni sisi kesho ni wewe. Kwa watu wa Narok, nawapenda nyote. Utuombee. Msijali, naamini itabadilika,” alisema.
Katika
chapisho jingine, alionyesha picha za kichwa cha mtafiti wake Bw Mudhune ambaye
alionekana kupaa majeraha wakati wa shambulio hilo.
Hapo
awali, mwanaharakati huyo wa kisiasa kijana alikuwa ameomba usaidizi akidai
kuwa baadhi ya watu wake wamejeruhiwa.
“Siwezi
kuwasiliana na yeyote anayeweza kuwasiliana na polisi kufika kwenye lami kutoka
Olulunga hadi Mau. Tafadhali,” Morara alisema katika chapisho moja.
Katika
chapisho lingine, alisema, “Ninahitaji usaidizi niko Narok kwa sasa baadhi ya
watu wangu wamejeruhiwa katika eneo la Ololulunga, Narok. Tafadhali saidieni wamejeruhiwa.”
Kwa
muda wa miezi michache iliyopita, mfanyabiashara huyo mwenye umri wa miaka 28
amekuwa akivuma kwenye mitandao ya kijamii na kwenye vyombo vya habari huku
akihusishwa pakubwa katika kukosoa serikali ya kitaifa na kaunti.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!