Jumapili
asubuhi, Waziri wa Usalama wa Ndani na Naibu Rais mteule Kithure Kindiki
alimpokea Rais William Ruto katika kaunti ya Kwale kabla ya sherehe za Mashujaa
Day.
Kindiki
alimpokea Mkuu wa Nchi katika makazi ya Kamishna wa Kaunti ya Kwale.
Naibu
rais mteule alijumuika na viongozi wengine akiwemo Katibu Mkuu wa Wizara ya
Mambo ya Ndani Raymond Omollo na Gavana Fatuma Achani miongoni mwa viongozi
wengine.
Hivi
leo, Oktoba 20, nchi inaadhimisha sherehe zake za 61 za Mashujaa.
Siku
hii ni ya kuwaenzi waliochangia pakubwa katika harakati za kupigania uhuru wa
Kenya kutoka kwa wakoloni.
Ni
siku ya kuenzi na kusherehekea ushujaa na kujitolea kwa watu wa Kenya
waliopigania uhuru wa nchi.
Usalama
umeimarishwa katika eneo kubwa la Pwani kutokana na sherehe hizo.
Pia
ni mara ya kwanza kaunti ya Kwale kuandaa hafla hiyo katika uwanja mpya wa
Kwale wenye uwezo wa kuchukua watu 10,200.
Wakati
wa hafla hiyo, mashujaa 142 watatambuliwa katika kategoria 14, ikijumuisha
michezo, hisani, umahiri na tamaduni za kiasili. Baadhi ya mashujaa watapata
kutambuliwa baada ya kifo baada ya mchakato wa uhakiki wa kina.
Kulingana
na katibu Mkuu wa Utamaduni na Urithi, Ummi Bashir, mashujaa waliochaguliwa
wametoa mchango mkubwa kwa jamii, mara nyingi wakihatarisha maisha yao ili
kunufaisha jamii zao, huku wengine wakipata kutambuliwa kimataifa kwa juhudi
zao.
Hafla
hiyo yenye mada kuhusu nyumba za bei nafuu, inatarajiwa kuvutia maelfu, akiwemo
Rais William Ruto, ambaye atawatunuku mashujaa 142 kwa michango yao kwa taifa.
Programu ya siku pia itaangazia ufunuo wa mipango muhimu ya serikali chini ya ajenda ya makazi ya bei nafuu.
Maadhimisho ya Siku ya Mashujaa yanajiri mwishoni mwa juma ambalo limeshuhudiwa tukio la kihistoria katika siasa za Kenya.
Mapema wiki hii, naibu wa rais RigathiGachagua alitimuliwa baada ya bunge la seneti kuidhinisha mashtaka mbalimbali yaliyotolewa dhidi yake.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!