Hivi leo, Jumamosi, Oktoba 19, wakili maarufu Ndegwa Njiru ambaye hivi majuzi alimwakilisha naibu wa rais aliyebanduliwa Rigathi Gachagua katika kesi yake ya kuondolewa ofisini kwake anafanya harusi ya kitamaduni.

Wakili huyo ambaye anajulikana sana kwa kuwawakilisha wateja katika kesi za kung’atuliwa mamlakani alitangaza mnamo Jumamosi asubuhi kwamba atafunga ndoa na mchumba wake Laureen katika harusi ya kitamaduni itakayofanyika katika eneo la Tala, kaunti ya Machakos.

Katika tangazo lake, Njiru alikiri mapenzi yake mazito kwa mchumba wake na zaidi akawaalika viongozi mbalimbali wakuu kwenye hafla hiyo.

“Leo barabara zote zinaelekea kaunti ya Tala Machakos kwa harusi yetu ya Kitamaduni. Ninakuthamini Laureen, wewe ni kipenzi cha maisha yangu,” Ndegwa Njiru alitangaza.

Aliongeza, “Karibu @skmusyoka @MarthaKarua @EugeneLWamalwa @HonKioni.”

Haya yanajiri siku moja tu baada ya wakili huyo kutoka nchi ya Kirinyaga kumwakilisha mwanasiasa Rigathi Gachagua wakati wa kesi yake ya kuondolewa madarakani.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Njiru miongoni mwa mawakili wengine wakiongozwa na Wakili Mkuu Paul Muite walitoa utetezi mkali sana kwa Gachagua katika seneti siku ya Jumatano na Alhamisi lakini haikutosha kuwazuia maseneta kumtimua naibu rais huyo ambaye amehudumu kwa miaka miwili pekee.

Maseneta mnamo  Alhamisi usiku waliunga mkono kuondolewa kwa Naibu Rais Rigathi Gachagua licha ya upande wa utetezi kuonekana kufanya vizuri katika kazi yao..

Maseneta waliidhinisha mashtaka matano kati ya 11 yaliyotolewa dhidi ya Gachagua.

"Seneti imeazimia kumuondoa afisini kwa kumwondoa madarakani MHE. Rigathi Gachagua, Naibu Rais wa Jamhuri ya Kenya. Kwa hiyo, H.E. Rigathi Gachagua akoma kushikilia wadhifa huo,” Spika Amason Kingi alisema.

Mashtaka yaliyoidhinishwa ni pamoja na; shtaka la maoni ya Wanahisa, mashtaka manne ya kuingilia Uhuru wa Majaji na mashtaka matano ya Sheria ya Uwiano na Uadilifu wa Kitaifa.

Pia walishikilia misingi ya sita na tisa kuhusu uhalifu chini ya Sheria ya Uwiano wa Kitaifa na Utovu wa Maadili Mkubwa.